Monday, November 21, 2011

NADI IKHWAN SAFAA, JUHUDI TAARAB ZAITEKA KISONGE



Wananchi wakiwa wametulia wakikongwa nyoyo zao na wasanii.

MAONESHO ya Taarab kushangilia maridhiano ya kisiasa Zanzibar, juzi yalihamia katika Uwanja wa Kisonge, ambapo vikundi vya nadi Ikhwan Safaa na Juhudi kutoika Chake Chake, Pemba viliwapa uhondo mashabiki wengi waliojimwaga kiwanjani hapo.

Tamasha hilo lililoandaliwa na Taasisi ya Swahili Performing Arts, lilivutia wapenzi wengi kutokana na nyimbo murua zilizoporomoshwa na waimbaji magwiji wa vikundi hivyo.

kundi la Juhudi ambalo lilikuwa la kwanza kupanda jukwaani, lilimudu vyema kuzikonga nyoyo za wananchi kwa nyimbo zao tamu kama vile 'Yatima', 'Zimekwisha enzi zako', 'Mshikamano' na Bora niombe' uliowavutia wangi.

Bibie Saada Mohammed Akighani wimbo wa Njangu.

Nalo kundi la Nadi Ikhwan Safaa liliamsha hisia za hadhira iliyofurika uwanjani hapo, kwa nyimbo za 'Wadhanifu' ulioghaniwa na mkongwe Sihaba Juma, 'Njangu' (Saada Mohammed), 'Hakika nnakupenda' (Ally Massoud)

Vibao vingine vilivyowazingua wapenzi ni 'Naomba kwako bibie'(Sameer Basalama),'Namuenzi'(Faudhia Abdullah), ambazo ziliwaibua washabiki kila mara katika viti vyao na kuungana pamoja kuserebuka.

Aidha wasanii wa vikundi hivyo kwa pamoja waliimba wimbo wa kusisitiza kuuendeleza muafaka na maridhiano kati ya wananchi wa Zanzibar, ukiwemo wimbo wa 'Maridhiano' (Faudhia Abdullah).

'Usiyalaumu macho' Mr. Wazera aliwakuna wananchi.

Msanii wa siku nyingi Sihaba Juma, alirudi tena jukwaani kugani wimbo 'Nnazama', klabu Wazera hajaonesha majojo majojo yake katika wimbo 'Usijalaumu macho', na Saada Muhammed akahitimisha onesho hilo kwa kibao 'Leo tena'.
Tamasha hilo limepangwa kuendelea tena Jumamosi ijayo katika ukumbi wa Ngome Kongwe, ambapo kundi la ' Unguja All Stars Taarab' na kikundi cha ngoma za asili 'Mkota' kutoka Mkoani Pemba vitatoa burdani mwanana. 

Ma mia ya watu walirindima katika uwanja wa kisonge.

Monday, November 7, 2011

KUMBWAYA LAWAPAGAWISHA NUNGWI


MKOTA wakilimwaga kubwaya, kabla ya wapenzi kuanza kupagawa

Sherehe za maridhiano na umoja wa kitaifa zilizoandaliwa na taasisi ya Swahili Center zinaendelea kwa kasi ambapo kwa Ijumaa iliyopita, vikundi vya Nyota ya Umoja (Maigizo,Nungwi) na Mkota Ngoma (Mkoani, Pemba) vilirindima katika kijiji cha Nungwi, Unguja.
Katika onesho hilo ambalo lilifanyika katika Uwanja wa Skuli ya Nungwi, Wilaya ya Kaskazini A, Mkoa wa Kaskazini Unguja, wapenzi wa fani za sanaa za maonesho kutoka sehemu mbali mabli waliliminika na kujimwaga katika burudani hizo zilizoanza saa 10 alasiri.
Kundi la Maigizo la Nyota ya Umoja, maarufu kwa michezo yao kama vile ‘Dhulma Kafara’ na ‘Masikini naye Mtu’, walitoa burudani safi kupitia mchezo wa ‘Mchelea Mwana Kulia’ uliobeba maudhui ya umuhimu wa ushirikiano wa kuyalinda maadili ya KiZanzibari ndani ya jamii.
Nalo kundi la Mkota Ngoma kutoka Mkoani, walikonga nyoyo za wapenzi wa Ngoma na asili kwa kupiga ngoma zao za Msembwe, Unjunguu na Kumbwaya. Wengi waliohudhiria shehere hizo walivutiwa sana na umahiri wa kundi hilo katika kuzicheza Ngoma hizo.
Katika kuutambulisha mradi huo kwa waliohudhuria onesho hilo, Mkurugenzi Mtendaji wa Swahili Center Bw. Kheri Abdalla Yussuf, aliwajulisha wapenzi hao wa sanaa za utamaduni kuwa dhamira ya mradi huo ni kuimarisha misingi ya umoja wa kitaifa nchini Zanzibar kupitia sanaa za utamaduni zenye burudani na mafunzo kwa jamii yote.
Wakati huo huo, aliyekuwa mgeni rasmi katika onesho hilo, Mhe. Bi Riziki Juma Simai (Mkuu wa Wilaya ya Kasakazi A) aliwataka wananchi wa Nungwi na wote waliohudhuria kuimarisha misingi ya umoja wa kitaifa kwa vitendo.
Mradi wa 100% Zanzibari (tafsiri; Mzanzibari asilimia mia moja) umekuwa ukifanya maonesho katika Mikoa ya Unguja na Pemba kufuatia kambi za kisanii zinazoshirikisha fani za Taarab, Ngoma za Utamaduni na michezo ya Kuigiza. Shangwe hizo zimekuwa zikifanyika kwa awamu katika sehemu mbali mbali ambapo kwa kipindi cha Nov 15-19 zitahamia katika Mkoa wa Mjini Maghribi.
Swahili Performing Arts Center (Kituo cha Sanaa za Maonesho cha Waswahili) ni taasisi ya iliyoanzishwa kwa dhamira ya kuchangia katika maendeleo ya sanaa za maonesho asilia za Zanzibar pamoja na zile za mwambao wa Waswahili kupitia uwezeshaji (wasanii), uzalishaji wa kazi za sanaa, maonesho na ushirikishaji jamii. Dira ya Swahili Center ni kuurejeshea hadhi utambulisho wa utamaduni wa Kiswahili.
Mradi wa 100% Zanzibari umedhaminiwa na Ubalozi wa Norway pamoja na kampuni ya mawasiliano ya Zantel.

Sunday, November 6, 2011

SWAHILI CENTER REPRESENTS CULTURE STAKEHOLDERS IN GHANA FORUM



Mkurgenzi wa Swahili Center, Kheri Jumbe (wa pili kutoka kulia) akiwa na Meya wa Jiji la Accrapamoja na wajumbe kutoka nchi za Nigeria, Ghana, Angola, Ghana, Afrika Kusini, Moroko na Senegal.

During the week of November 7-10, the Zanzibar-based Swahili Performing Arts Centre Managing Director, Kheiri Jumbe, attended the African Cultural Capital’s City Forum on Culture and Development, in Accra, Ghana.

The Isles was invited on merit of both the tangible and intangible cultural assets present in Stonetown. In a telephone conversation on Friday, Jumbe told the ‘Daily News on Saturday,’ “I am here to attend a forum on strategies towards making culturally active African cities to be recognised by UNESCO as being that.” According to Jumbe the aim of the meeting was to strategise on ways to infuse culture and the creative industries agendas at the heart of national development policy.

Cultural leaders from several African countries got the chance to explore development policies in their respective countries in relation to funding modalities and programming approaches. Countries represented at the forum, which took place between Monday and Thursday this week were Cameroun, Morocco, South Africa, Nigeria, Mozambique, the hosts Ghana and Tanzania.


Kheri akitoa mada kuhusu ustawi wa sanaa na utamaduni wa Zanzibar ka mtazamo wa Swahili Center

The Mayor of Accra, Alfred Oko Vanderpuije, was the host of the 4-day event, which was organised by the City of Accra, The Arterial Network, UNESCO, The Goethe Institut and Agenda 21 of Spain. “My personal ambition and that of the Swahili Centre as stakeholders in culture in Tanzania is to develop ways in which the competitiveness of culture in the context of its productivity can be enhanced for the benefit of the local economy,” Jumbe replied when asked about the purpose of his participation.

He further explained that many studies conducted on the social and economic impact of cultural and creative industries have shown “positive contribution towards social cohesion, economic development and poverty reduction.” UNCTAD data shows that cultural and creative industries worldwide grew an average of 8.7 per cent annually.

However, Jumbe contended in many developing countries culture is not mainstreamed into development policies, despite “UNESCO recognising it as a vector for development and promoter of international co-operation.” As a result, there is generally lack of long-term, co-ordinated effort and funding in the sector in many developing countries. Inevitably, most support for culture in developing countries comes from international donors and multinational corporations, he maintained.

Kheri na mwenyeji wake Philibert wakitembelea kumbukumbu ya Rais wa Kwanza wa Ghana Marehemu Kwame Mkrumah

These only tend to concentrate on short-term and highly visible projects that are usually insufficient to render the sector viable.